Monday, 15 September 2014









EBOLA NI SHIDAH!!

Kuna mtu aliekwenda kanisani
Jumapili akatoa ushuda kuwa
alikuwa na ebola na Mungu
akamponya. Alipomaliza akataka
ampe 'mic' mtu anayefuata,
jamaa akakataa.

jamaa:(Mh! ebola?)Sina ushuhuda mpe
pastor.

Pastor:(mh amepona kweli huyu)Mimi sihusiki na shuhuda,
mpe senior pastor.

Senior pastor:(Hata mtoto mdogo hakubali)Ndugu katika kristo.
Mic ni ya kwako. Ni zawadi kutoka
kwa kanisa. Nenda nayo
nyumbani.

EBOLA ni shidah

MWALIMU MKUU NA WANAFUNZI WAKE WOTE MACHIZI

Haha eti mmenibania kunipigia kura sasa nimepandishwa mshahara kutoka 80k hadi 10k msionipigia ntawapiga mateke wote haya sura ya kazi sasa

mwalim wa history akawauliza
wanafunz
mwl:eehe! ni nani aliyemuua chifu
mkwawa?
mwanafunz 1:aka! sio mimi
wa 2:wallah! siusiki
wa3:kwanza mi jana cjaja shule!
mwl alipoona wanafunz wote ni
vilaza akaamua kumuita mkuu wa
shule,mkuu wa shule alipoenda
akawauliza lile swali kwa
vitisho,mambo yakawa vilevile
ndipo mkuu wa shule alipomuita
mwl pemben na kumnong'oneza
"lakini una uhakika muuaji yupo
darasa hili?"

NDOA IMEINGILIWA NA NJEMBA

Waifu wa jamaa mmoja alikuwa akisumbuliwa sana na njemba fulani iliyokuwa ikimtaka kila siku, hatimae waif akamwambia mumewe. Mume akamwambia mkewe, "Unajua watu kama hawa dawa yao ndogo tu,we mkubali tu, ila mwambie aje mlale hapa kwetu, mi ntajificha uvunguni na panga. Akisha ingia ukiona kamaliza kuvua nguo we ning’iniza mkono anza kuuchezesha, mi nikiuona ntatoka uvunguni na kumfunza adabu".
Mamaa akafuata masharti ya mumewe na hatimae akaweza kuirubuni njemba hadi wakaingia chumbani, mume akawa tayari na panga uvunguni mwa kitanda anangojea signo.
Jamaa alipovua shati, mke alishangaa kuona njemba ina makovu makubwa kifuani na mgongoni akaamua kuuliza, "Hee jamani mbona una makovu hivyo?", Njemba huku ikiendelea kuvua suruali ikajibu," Niwe mkweli mie nina pepo la kupenda wake za watu, waume wengi wamekuwa wakipanga kunifumania, nimeshafumaniwamara kumi na tisa, na wote walionifumania nimewaua". Mamaa akbaki kuduwaa tu. Jamaa alipomaliza kuvua nguo mdada akaanza kuning’iniza mkono ili mumewe atoke uvunguni, mume kabana kimya, kila jitihada za mdada kupunga mkono hazikupata majibu, mpaka njemba ikamaliza shughuli zake akatokomea.Ndipo mume akatoka uvunguni jasho linamtoka,"Sasandio umefanya nini mume wangu? Umeacha nimeshindwa kufanya lolote, kwanini hukutoka jamanii?" . Mume akajibu kwa ukali," We we we, mwenyewe umesikia kasha ua 19 unataka niwe wa ishirini? nauliza unataka niwe wa 20 kusudi muendelee na uasherati wenu?